<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rdf:RDF xmlns="http://purl.org/rss/1.0/" xmlns:rdf="http://www.w3.org/1999/02/22-rdf-syntax-ns#" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/">
<channel rdf:about="http://hdl.handle.net/123456789/15717">
<title>Doctor of Philosophy in Kiswahili.</title>
<link>http://hdl.handle.net/123456789/15717</link>
<description/>
<items>
<rdf:Seq>
<rdf:li rdf:resource="http://hdl.handle.net/123456789/18769"/>
<rdf:li rdf:resource="http://hdl.handle.net/123456789/15681"/>
<rdf:li rdf:resource="http://hdl.handle.net/123456789/15676"/>
</rdf:Seq>
</items>
<dc:date>2026-04-05T18:46:46Z</dc:date>
</channel>
<item rdf:about="http://hdl.handle.net/123456789/18769">
<title>TATHMINI LINGANISHI YA USAWIRI WA USHUJAA KATIKA TENDI ZA FUMO  LIYONGO, MIKIDADI NA MAYASA NA SWIFA YA NGUVUMALI</title>
<link>http://hdl.handle.net/123456789/18769</link>
<description>TATHMINI LINGANISHI YA USAWIRI WA USHUJAA KATIKA TENDI ZA FUMO  LIYONGO, MIKIDADI NA MAYASA NA SWIFA YA NGUVUMALI
EVANS OMBENG’I NYACHOI
Utafiti huu ni tathmini ya usawiri linganishi wa ushujaa katika tendi za Fumo Liyongo, &#13;
Mikidadi na Mayasa na Swifa ya Nguvumali. Madhumuni ya utafiti huu ni kumtambulisha &#13;
shujaa kwa vigezo vya ushujaa wa Kiafrika katika tendi teule za Kiswahili, kutathmini &#13;
mchango linganishi wa mazingira katika kusawiri ushujaa katika tendi teule na kubainisha &#13;
kiulinganifu matumizi ya mbinu za utunzi katika kusawiri ushujaa katika tendi teule.  Uteuzi &#13;
wa mada ya utafiti uliongozwa na kuwepo kwa pengo la kiusomi. Hata ingawa tafiti nyingi &#13;
zimefanywa kuhusiana na swala la ushujaa, mtafiti hajaweza kutagusana na utafiti &#13;
uliochunguza ulinganishi wa ushujaa katika tendi teule za Utendi wa Fumo Liyongo, Utendi &#13;
wa Mikidadi na Mayasa na Utendi wa Swifa ya Nguvumali. Utafiti huu uliongozwa na &#13;
nadharia tatu. Nadharia ya kwanza ni Mithiolojia iliyoasisiwa na Raglan (1936) na Rank &#13;
(1909) na kuendelezwa na Okpewho (1979) na Mulokozi (2002). Nadharia ya Mithiolojia &#13;
imeorodhesha sifa bainifu za shujaa wa Kiafrika ambazo shujaa wa Kiafrika anafaa kuwa &#13;
nazo katika tendi. Nadharia ya pili ni Ujumi Mweusi ya Zirimu (1971). Nadharia hii &#13;
inapendekeza fasihi ya Kiafrika ihusishe Uafrika na mazingira ya Kiafrika katika kusawiri &#13;
ushujaa. Nadharia hii inalenga kuonyesha hali ya kujivunia Uafrika. Nadharia ya tatu ni &#13;
Umaumbo ya Shyklovsky ( 1904) na kuendelezwa na Roman ( 1919). Nadharia ya Umaumbo &#13;
inashikilia kuwa kazi za fasihi ziweze kuandikwa kwa sifa bainifu za umbo maalumu na &#13;
zitumie mbinu mahususi za utunzi katika kufikisha ujumbe wa kifasihi. Utafiti huu ulikuwa &#13;
wa maktabani. Maktaba mbalimbali yakiwemo ya intaneti yalitumika. Kundi lengwa la utafiti &#13;
huu, lilikuwa tendi za Kiswahili, ambapo kimaksudi mtafiti aliteua tendi tatu ambazo ni &#13;
Utendi wa Fumo Liyongo, (Kijumwa, 1913) Utendi wa Mikidadi na Mayasa, (Bashir 1972), &#13;
na Utendi wa Swifa ya Nguvumali, (Ismaili 1968). Data imeandikwa kwenye nakala ngumu &#13;
na pia kwa tarakilishi. Data ilikusanywa kwa njia ya uchanganuzi wa yaliyomo kwa &#13;
kuzisoma tendi zenyewe na kazi mbalimbali zilizohusu suala la ushujaa. Uchanganuzi wa &#13;
data ulikuwa kwa njia ya maelezo ambapo data ilieandikwa, ikachujwa na kufafanuliwa. &#13;
Matokeo ya utafiti yamewasilishwa kwa njia ya maandishi. Utafiti huu umemtambulisha &#13;
shujaa kwa vigezo vya shujaa wa Kiafrika katika tendi teule, na uligundua kuwa, si kila &#13;
shujaa wa tendi teule za Kiswahili uafiki vigezo vya kumtambulisha shujaa wa Kiafrika. &#13;
Mtafiti ametathmini mchango linganifu wa mazingira, na kuamua kuwa mazingira yana &#13;
mchango mkubwa katika kumjenga shujaa katika tendi teule za Kiswahili. Kiulinganifu, &#13;
utafiti uligundua kuwa, mbinu za utunzi zina nafasi kubwa katika kusawiri ushujaa. Mbinu &#13;
nyingi zilitumika katika tendi zote ila tu mbinu za Ndoto na Ngomezi, ambazo zilitumika &#13;
katika baadhi ya tendi. Matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuwa ya muhimu kwa jamii ya &#13;
wasomi katika urejeleaji wa dhana ya ushujaa na kuzua mtazamo mpya wa usawiri wa &#13;
ushujaa kwa kulinganisha ushujaa katika tendi teule. Utafiti huu ni daraja kwa watafiti wa &#13;
baadaye na ni nyongeza kwa tafiti ambazo zimefanywa kuhusiana na suala la ushujaa katika &#13;
tendi za Kiswahili.
</description>
<dc:date>2025-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</item>
<item rdf:about="http://hdl.handle.net/123456789/15681">
<title>TATHMINI YA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA UWASILISHAJI WA HABARI ZA MAZINGIRA KATIKA GAZETI LA TAIFA LEO LA KENYA</title>
<link>http://hdl.handle.net/123456789/15681</link>
<description>TATHMINI YA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA UWASILISHAJI WA HABARI ZA MAZINGIRA KATIKA GAZETI LA TAIFA LEO LA KENYA
NELLY NZULA KITONGA
Utafiti huu unahusu tathmini ya matumizi ya lugha katika uwasilishaji wa habari za&#13;
mazingira katika gazeti la Taifa Leo nchini Kenya. Gazeti la Taifa Leo huwasilisha habari&#13;
kwa wasomaji kwa lugha ya Kiswahili. Lugha ya Kiswahili inatambuliwa na Katiba ya&#13;
Kenya kama lugha ya taifa na pia lugha rasmi sambamba na lugha ya Kiingereza.&#13;
Mazingira ni suala mtambuko na nyeti kitaifa na kimataifa. Mazingira yanaathiri maisha&#13;
ya kila kiumbe kila siku kwa njia moja au nyingine. Inatarajiwa kwamba, kwa vile vyombo&#13;
vya habari, Gazeti la Taifa Leo likiwemo, vimetwikwa jukumu la kuwapasha wanajamii&#13;
yale yanayoendelea duniani kuhusiana na mazingira, vitafanya hivyo kwa namna ambayo&#13;
itawawezesha watu kufahamu umuhimu wa mazingira na hivyo kuingiliana nayo kwa njia&#13;
chanya. Hoja hii inatokana na imani kwamba mtu huthamini na kutunza kile anachofahamu&#13;
thamani yake. Uchunguzi huu ulinuia kubainisha iwapo matumizi ya lugha katika kueleza&#13;
habari za mazingira kwenye gazeti la Taifa Leo hufanikisha mawasiliano. Uchunguzi huu&#13;
ulidhamiria kutimiza malengo yafuatayo: kuchanganua vipengele vya lugha&#13;
vinavyoteuliwa na waandishi wa habari katika kuripoti habari za mazingira katika gazeti&#13;
la Taifa Leo, kutathmini mtindo wa uwasilishaji wa habari za kimazingira na kubainisha&#13;
ujumbe uliowasilishwa na waandishi wa habari katika gazeti la Taifa Leo. Nadharia&#13;
zilizotumika katika utafiti huu ni Nadharia ya Uchanganuzi Usemi (NUU) iliyoasisiwa na&#13;
Michel Foucault (1928) na baadaye ikaendelezwa na Norman Fairclough (1989) na&#13;
Nadharia ya Umtindo (NU) ambayo iliasisiwa na Geoffrey Leech (1965-1966) na&#13;
ikapaliliwa na Simpson (2004). Utafiti huu ulifanyika maktabani ambapo taarifa kuhusu&#13;
habari za mazingira zilizochapishwa katika gazeti la Taifa Leo zilichanganuliwa. Magazeti&#13;
ya Taifa Leo yaliyochapishwa kuanzia Januari 2021 hadi Machi 2022 yaliteuliwa kwa&#13;
kudhamiria, hususan yale yaliyokuwa na habari kuhusu mazingira. Data ilikusanywa kwa&#13;
kudondoa matumizi ya lugha, mtindo uliotumiwa katika uwasilishaji wa taarifa za&#13;
mazingira kutoka magazeti ya Taifa Leo teule pamoja na aina na dhima za ujumbe&#13;
uliojitokeza katika habari hizo. Utafiti huu ulichanganua matini 270 kutoka kwa magazeti&#13;
ya Taifa Leo yaliyoteuliwa kimaksudi. Matini hizi ni zile ambazo zilifafanua taarifa&#13;
zinazohusiana na mazingira. Data iliyokusanywa katika utafiti huu ilikuwa ya kithamano.&#13;
Data ya kithamano ilikuwa zile habari zilizofafanua masuala ya mazingira katika gazeti la&#13;
Taifa Leo. Data ya kithamano ilichanganuliwa kwa njia ya maelezo kwa kuzingatia&#13;
mihimili ya nadharia teule. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kwa maelezo, jedwali na&#13;
takwimu. Inatarajiwa kwamba matokeo ya utafiti huu yatafaidi wanafunzi, watafiti,&#13;
wanaharakati wa kimazingira, taaluma za Uchanganuzi Usemi, Umtindo na Pragmatiki,&#13;
wanahabari, wachapishaji wa habari katika magazeti, na wasomaji wa habari hizo.&#13;
Umuhimu wa Kiswahili kama wenzo wa mawasiliano pia umeangaziwa.
</description>
<dc:date>2023-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</item>
<item rdf:about="http://hdl.handle.net/123456789/15676">
<title>MUUNDO NA RUWAZA YA VIVUMISHI KATIKA TUNGO ZA KIIMENTI</title>
<link>http://hdl.handle.net/123456789/15676</link>
<description>MUUNDO NA RUWAZA YA VIVUMISHI KATIKA TUNGO ZA KIIMENTI
KENNETH KINYUA THURANIRA
Utafiti huu ulishughulikia muundo na ruwaza ya kivumishi cha lahaja ya Kiimenti&#13;
kinapotumika katika tungo za Kiimenti. Kiimenti ni lahaja mojawapo ya lugha ya Kimeru&#13;
inayozungumzwa katika kaunti za Meru na Tharaka Nithi. Lahaja hii haijafanyiwa utafiti&#13;
mwingi. Kwa hivyo, utafiti huu ni jitihada za kuongezea maarifa katika lahaja hii.&#13;
Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa kubainisha aina za vivumishi katika lahaja ya&#13;
Kiimenti; kuchunguza miundo ya vivumishi vya Kiimenti na jinsi usarufi&#13;
unavyowakilishwa katika maumbo ya vivumishi; kupambanua ruwaza za usarufi katika&#13;
vivumishi vya Kiimenti na kutathmini sheria za mpangilio wa vivumishi katika tungo za&#13;
Kiimenti. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Sarufi Geuza Umbo Zalishi (Chomsky,&#13;
1957; 1965) na Nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia (Hooper, 1976). Nadharia ya Sarufi&#13;
Geuza Umbo Zalishi ilisaidia kuchanganua maumbo ya vivumishi kimofemiki huku&#13;
miundo ya nje na ndani ya vivumishi husika ikichunguzwa. Vivumishi vya Kiimenti&#13;
hupitia michakato mingi ya kifonolojia vinapodhihirisha muundo wa nje kutoka muundo&#13;
wa ndani. Nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia ilitumika kuchunguza michakato hiyo na&#13;
sheria zinazohusika. Uchunguzi wa nyanjani na maktabani ulifanyika. Nyanjani, utafiti&#13;
ulifanywa katika wadi ya Abothũgũchi ya Magharibi katika kaunti ndogo ya Meru ya&#13;
Kati. Mbinu ya sampuli makusudi ilitumiwa kuteua eneo la utafiti na wasailiwa&#13;
walioshirikishwa katika utafiti huu. Walengwa wa utafiti huu walikuwa wazungumzaji&#13;
wazawa wa lahaja ya Kiimenti ili kuhakikisha uthabiti wa data. Mtafiti alihudhuria&#13;
mikutano ya machifu, kanisa na ya wazazi shuleni ili kukusanya data ya vivumishi&#13;
ambayo ilichanganuliwa. Mbinu za utafiti zilizotumiwa ni kurekodi mazungumzo ya&#13;
wasailiwa katika mikutano hii kwa kutumia kalamu na karatasi pamoja na kinasa sauti&#13;
cha rununu. Aidha, tasnifu, makala mahsusi na vitabu hasa vya hadithi katika lahaja ya&#13;
Kiimenti na vingine vilivyohusu mada ya utafiti huu vilisomwa katika maktaba za vyuo&#13;
vikuu vya Kenyatta, Nairobi, Moi, Egerton na Chuka. Kazi zaidi zilisomwa katika&#13;
maktaba ya Wizara ya Elimu iliyoko jijini Nairobi ambapo tasnifu nyingi za vyuo vikuu&#13;
mbalimbali zimehifadhiwa. Data ya vivumishi vya Kiimenti iliyopatikana&#13;
ilichanganuliwa kwa kupanga aina mbalimbali za vivumishi katika majedwali na&#13;
kuondoa uradidi uliojitokeza. Kisha vivumishi husika vilifanyiwa unukuzi wa kifonetiki&#13;
na kutafsiriwa. Aidha, vilichanganuliwa ili kuamua utendakazi wa kisarufi ulioainishwa.&#13;
Hatua nyingine ilihusu kupangilia sentensi zenye mpangilio sawa wa vivumishi pamoja&#13;
na kuzifanyia unukuzi wa kifonetiki. Kisha zilitafsiriwa na sheria kuandikwa zilizodhibiti&#13;
kila ruwaza ya vivumishi katika sentensi. Utafiti ulibainisha kuwa kivumishi cha&#13;
Kiimenti huwasilisha muundo mahsusi wenye mofimu zinazotekeleza kazi za kisarufi.&#13;
Inatarajiwa kwamba utafiti huu utakuwa mchango mkubwa wa kiisimu kwa kuwasaidia&#13;
wanafunzi, walimu na watafiti wengine wakichunguza lugha za kiasili. Pia, utafiti&#13;
utasaidia katika uhifadhi wa lahaja ya Kiimenti kwa vizazi vijavyo.
</description>
<dc:date>2023-01-01T00:00:00Z</dc:date>
</item>
</rdf:RDF>
